Translate

Friday, June 26, 2020

BRYAN DECON MUIGIZAJI WA FILAMU YA JESUS

BRIAN DECON MUIGIZAJI WA FILAMU  YA JESUS




Filamu Ya JESUS:
Ni Filamu iliyogusa maisha ya watu wengi Duniani kiasi kwamba wakasahau kuwa Mwigizaji wa Filamu hiyo hakuwa YESU halisi, ila ni Muigizaji na ni Binadamu wa kawaida kama wengine.

Filamu hii iitwayo “JESUS” Imeigizwa Nchini Israel na Muigizaji kutoka nchini Uingereza aitwaye Brian Deacon mnamo Mwaka 1979 ambapo kiuhalisia hakuwa Mkristo lakini Uigizaji huo ulimfanya Aokoke mara baada ya kuitazama filamu hiyo akiwa na miaka-30 na kubadili dini na kuwa Mkristo. 
 
 HISTORIA YA DEACON:
Jina lake kamili Msanii huyu anaitwa Brian Deacon alizaliwa Oxford Nchini Uingereza mwaka 1949 akiwa ni mtoto wa pili kutoka katika familia ya Deacon,

(Baba yake) ambaye alikuwa ni Fundi wa kutengeneza magari (Mechanic) na Mama yake akiwa ni Nesi wa hospitali (Nurse)

Ndoa ya kwanza ya Brian na mkewe Bi. Lenska, ilivunjika ambapo walifanikiwa kupata mtoto wa kike aitwaye Lara Deacon, na ndoa yake ya pili alifunga na Natalie Bloch Mnamo mwaka-1998 ambaye yupo naye hadi hivi sasa.

Bwana Brian alipitishwa katika Mchujo wa Waigizaji zaidi ya 1,000 ambao walifanyiwa mahojiano huku-260 wakijaribishwa kuigiza (screen test) na yeye akiwa ni Mwingereza pekee kufaulu mtihani huo na kuchaguliwa kuwa muhusika mkuu (Sterring).

Filamu hii ya (JESUS) imenukuliwa katika maandiko matakatifu ya Kitabu cha LUKA, ambapo Bw Brian anasema ilinichukua zaidi ya mara-20 kwa wiki3 kusoma kitabu cha Luka Mtakatifu pekee, ambapo kusoma huko ilisaidia kumfahamu vyema Yesu Kristo ni mtu wa aina gani, ikanipa nguvu na Ujasiri wa kuigiza filamu hii” alisema_Bw_Deacon  

Katika uigizaji wa Filamu hii ya JESUS, ulichukua zaidi ya miezi-7 kurekodiwa, kuanzia majira ya alfajiri mpaka kiza kilipozama, na miezi mingine-7 kurekodiwa 

na Bw_Brian anasema:
“katika uigizaji huo hakuna aliyechoka kwani Waigizaji wote walikuwa wakipokea nguvu ya ajabu kutoka juu (Mbinguni) na hivyo kuifanya kazi hiyo kuwa nyepesi hadi kukamilika kwake

Alisema.
Baada ya Filamu hiyo ya 'JESUS' Bw. Brian alirudi kuigiza Majukwaani na kwenye runinga ambapo kwa miaka zaidi ya 30 hadi hivi sasa tokea kutoka kwa filamu hiyo, tayari imeshatazamwa na watu zaidi ya milioni-133. (hii ni kwa mujibu takwimu za mwaka-2001) ambapo wote walibadilisha maisha yao na kuokoka mara baada ya kuitazama filamu hiyo.

Amesema kabla ya kuchaguliwa mtihani wake wa kwanza ulikuwa kutoka kwa wakala wake aliyemvunja moyo kwakumweleza hadhani kama yeye(Brian)atafaa kwenye kumwigiza Yesu,lakini anasema alifanikiwa,baada ya hapo akawa na wakati mgumu kutoka kwa watu ambao kila mmoja alikuwa anajaribu kumweleza jinsi anavyotakiwa kuigiza,sauti yake na mambo mengine,ingawa yeye alisema nitatumia sauti yangu na maelezo kutoka kwa muongozaji.


Siku nyingine waliokuwa wakiigiza kama wanafunzi wa Yesu wapatao 12 wakiwa ndani ya basi walikuwa wamepanga kugoma kutokana na malipo waliyokuwa wakipata cha ajabu Brian anasema director alikuja kumuomba yeye(Brian)azungumze nao warejee kazini akashangaa akamwambia mimi sio Yesu ni Brian Deacon,akaamua kuzungumza nao,baada ya masaa 36 walikubali kurudi kuendelea na kazi

Amesema mtihani mwingine ni siku alipokuwa hotelini Tel Aviv ghorofa ya 18 usiku mara kukawa na moto hotelini hapo baada ya mwingereza mmoja aliyekuwa akivuta sigara kusahau kuizima hivyo kusababisha moto,lakini anasema bahati nzuri hakuna aliyejeruhiwa ila walifanya kazi siku inayofuatia muda mrefu bila muongozaji kujali kwamba hawakulala vyema usiku.

Amesema siku hiyo mmoja wa waigizaji anayeitwa Tom Panella alianzisha mada kwa kusema moto uliokuwa umetokea ni hila za shetani,na kusababisha mjadala wa muda mrefu ni vipi shetani anahusishwa kwenye swala hilo lakini jibu likawa,shetani hataki filamu hiyo irekodiwe ndio maana analeta hila zake.haikuwa kazi rahisi kurekodi filamu hiyo na pia si ujuzi wa kufurahia,baada ya kumaliza kurekodi kwa takribani miezi 18 ilianza kuonyeshwa kwa baadhi ya watu na ndipo hata yeye kwa mara ya kwanza akaona ni kwa jinsi filamu hiyo ilivyonanguvu,ukweli na kugusa mioyo ya watu



Brian anawaambia watu kwamba yeye ni mwigizaji tu na sio Yesu kama watu wengine na kuwataka watu hao kujua hivyo ambapo anasema ameendelea kupata barua mbalimbali za kumpongeza na kumshukuru kwa kazi nzuri aliyofanya kwenye filamu hiyo,ambapo kwa upande wake anasema anayo nakala ya filamu hiyo kwenye maktaba yake nyumbani kwao Uingereza,ambapo kwa takribani miaka 20 filamu hiyo imekuwa ikitazamwa duniani kote na kubadilisha maisha ya watu

No comments:

Post a Comment

SIXBERTY MANSON POSTS

Mona Lisa

  MONALISA                              LA GIOCONDA                          By Sixberty Manson  A picture by Sixberty Manson  MEET THE REAL...

ZILIZOTAZAMWA ZAIDI