Translate

Wednesday, March 4, 2020

NJE YA BOX ( KUCHEPUKA)


OUTSIDE BOX (NJE YA BOX)
KUCHEPUKA 
By Sixberty Manson 




Moral standard za ndoa sasa zimeshuka kiasi kwamba
si ajabu tena kuona bibi harusi na vazi la harusi huku ana mimba kubwa!

Karibu watu wote wanaokamatwa na suala la kutokuwa waaminifu katika ndoa zao hukubali kwamba ni kweli wamekosea na wengine husema ni shetani tu aliwaingia.
Tafiti zinaonesha kwamba katika jamii yoyote duniani asilimia 25 ya wanaume huchepuka nje ya ndoa zao na asilimia 10 ya wanawake hukiri kuchepuka kwenye ndoa zao hii haina maana wanandoa wenzao hujua suala ni kwamba huwa wanakiri kwamba wamewahi kutoka nje ya ndoa zao.

NINI HUSABABISHA WENGI KUCHEPUKA

Kutoridhika na ndoa zao idara zote na kuanza kutafuta mtu wa nje ili kuridhishwa.

Matatizo ya familia.
Wengine hujikuta amempenda mtu mwingine.

Kutengana kwa muda mrefu mume na mke inaweza kuwa masomo au kazi nk.

Kushuka kwa kiwango cha kiroho cha wanandoa.
Kuhitaji kuridhishwa zaidi kimapenzi; kuna watu wana libido la ajabu!
Kutafuta Kujiamini na kutambuliwa kwamba yeye ni nani katika jamii
Kuikata kweli ya Neno la Mungu.

Ukaidi na uhuni.
Hitaji la kupendwa baada ya kutelekezwa.
Kuzaliwa mtoto wa kwanza katika ndoa; Feelings za kumpa mume huhamia kwa mtoto na wanandoa hujikuta wapo emotionally distant.


NINI HUSABABISHA WENGI KUGOMA KUCHEPUKA.

Kujitoa kwa ndoa na kulinda ahadi na agano (covenant)
Kuaminiana kwa wanandoa.

Sababu ya dini yaani wokovu (uhusiano binafsi wa mwanandoa na Mungu).

Kuogopa matokeo ya kuchepuka kama vile magonjwa (UKIMWI) na crisis zingine.

Kujifahamu na kukomaa kiakili na Kujiamini.

Kupenda mke na watoto na kuwapa heshima iliyotukuka na kuishi kwa mfano kimatendo na kimaneno.

Uadilifu (moral standard)


Linapokuja suala la ndoa au mahusiano huu usemi wa kingereza usemao “How Far is too Far’ una maana kwamba je, ni namna gani au utajuaje au ni kufanya kitu gani hueleza kwamba hujawa mwaminifu kwa mke wako au mume wako.
Kujua hujawa mwaminifu ni pale kile unafanya au yale unaongea na mwanaume mwingine au mwanamke mwingine huwezi kumwambia mke wako au mume wako.

MFANO
Jeffy ni kijana smart sana kazini na nyumbani na kwa sasa anajiona yupo bored nyumbani hasa kutokana na yale yanayoendelea katika maisha na mkewe Jane.
Hivyo anaamua kutaniana na kujihusisha zaidi na mwanamke anayeitwa Lily ambaye ni mfanyakazi mwenzake ofisini.
Katika kutaniana kwao urafiki unazaliwa na wanajikuta wanakuwa muda mwingi pamojana kuvutiana zaidi; sasa iwe lunch, au kinywaji baada ya muda wa kazi Jeffy yupo na Lily.

Baada ya siku na miezi kadhaa wanajiona karibu zaidi na Jeffy anajikuta anamwambia Lily siri zake za nyumbani na mkewe na Lily naye anamwambia Jeffy siri ambazo hajawahi kumwambia mtu yeyote.
Sasa wakikutana wakiwa wawili ni kupeana kisses na hugs kwa kwenda mbele ingawa bado hawajavuliana nguo.
Yote haya yanapotokea Jeffy hajamweleza mke wake.

Je, Jeffy amekuwa si mwaminifu kwa mke wake? Au kwa ndoa yake?
Je ungekuwa wewe ni Jeffy ungemwambia mke wako huo urafiki na mwanamke Lily?
Au ungekuwa ni mwanamke Lily ambaye umeolewa Ungemwambia mume wako urafiki wako na Jeffy?

KUKOSA UAMINIFU KATIKA NDOA NI NINI?
Kukosa uaminifu katika ndoa ni utendaji unaoanzia ndani ya moyo kuvunja trust na ahadi ya ndoa kimwili, kiakili, kimawazo na kihisia na siri zote za ndoa.
Ni kuvunja agano na pia ni kumsaliti mwenzi wako.

Je, unaweza kujihusisha na mtu mwingine nje ya ndoa kihisia na ukabaki mwaminifu kwa ndoa yako?

Jibu ni hapana kwani ulipokubali kuoana naye ulikubali kwamba mtakuwa mwili mmoja (one flesh); kuwa mwili mmoja ni pamoja na emotions, feelings, mawazo na maisha yote ya ndoa kwa ujumla.
Unatakiwa kuwa kwa mwenzi wako kimawazo na kimwili.

Uzinzi wa emotions upo serious sawa na ule wa kimwili
“Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Usizini'.
Lakini mimi nawaambia: kwamba ye yote amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.
(Mathayo 5:27-28)

Uzinzi ni sehemu ya infidelity ( kukosa uaminifu katika ndoa) infidelity ni kutimiza hitaji la mwili na hisia nje ya ndoa wakati adultery ni sex nje ya ndoa.

Kama ninyi ni wachumba na mmoja si mwaminifu huo unaitwa ni uasherati na ni vizuri kuachana kwani mchumba asiyemwaminifu huja kuwa mwanandoa asiyemwaminifu.

Washauri wa mambo ya ndoa wanafahamu fika kwamba katika matatizo mengi ya wanandoa suala la kukosa uaminifu (infidelity) kawaida ni nusu ya matatizo yote katika ndoa.

Ujue au usijue kwamba kuna kuchepuka metokea katika ndoa yako ukweli unabaki kwamba matokeo ya mwanandoa mmoja kuchepuka nje ya ndoa yake ni mabaya sana kwa yeye mwenyewe, ndoa yake na huweza kuleta crisis kubwa ya familia na hata jamii kama si taifa.
Fikiria suala la UKIMWI tu.

VITUKO VYA KUCHEPUKA NJE YA NDOA.

Kawaida mwanandoa anayechepuka akikamatwa na kupewa talaka mara nyingi hawezi kuoana na yule aliyekamatwa naye.
Hivyo kama upo kwenye affair na mwanaume wa mtu au mke wa mtu kumbuka kwamba hupati point yoyote au kukuongezea uwezekano wa yeye kuoana na wewe ikitokea amepata talaka.

Affair ni dalili za huzuni iliyopo kwa wanandoa na maana yake mmoja anakosa hisia sahihi kwa mwenzake na matokeo yake husukumwa kuchepuka nje na akishachepuka huongeza matatizo mengine zaidi ya ndoa kama vile kuchelewa kurudi nyumbani, matumizi ya pesa na magonjwa.

Si sahihi kwamba kuwa na affair ni kupata great sex, kutoka nje ni vibaya kwa sababu ni kweli kwenye ndoa kuna great sex na "we need to spread the word" kwamba kwenye ndoa sex ni tamu zaidi.

Si kweli kwamba mwanandoa anayechepuka hufuata mwanamke mrembo zaidi kuliko aliyekwenye ndoa yake au mwanaume maridadi zaidi kuliko aliye kwenye ndoa yake, wengi huvutwa na feelings zile wanakosa ndani ya ndoa zao.

Affair nyingi zina base kwenye urafiki na kuungana kihisia na sharing ya siri na feelings mbalimbali na wakati mwingine sex huwa si sababu ya kuwa na affair bali urafiki wa karibu kwa jinsia tofauti.

Tamaduni nyingi humwangalia vibaya mwanamke kuliko mwanaume linapokuja suala la mwanandoa kuchepuka nje.

Kubwa zaidi ni kwamba uwezekano wa kutolewa talaka ni pale mwanamke akionekana ametoka nje ya ndoa (cheating) kuliko mwanaume akitoka nje ya ndoa.


DALILI KWAMBA ANACHEPUKA.

Dalili za mwanaume anayechepuka

1. ANATUMIA MUDA MWINGI NJE NA NYUMBANI
Huwezi kuwatumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja na kila mmoja ukampa muda sawa, it is impossible.
Wengi huanza kubadilika na kukwepa kuwepo nyumbani na mke wake hata kabla ya affair (astray).
Mwanaume kutumia muda mwingine nje ya nyumbani haina maana kwamba ana-cheat bali inaweza kuwa dalili kwamba ana cheat hasa kukiwa na dalili zingine.
Hata hivyo ukigundua mapema unaweza kuzuia na kuepuka maumivu ya cheating.
Wakati mwingine “hawa wanaume” huwafunga kamba wake zao kwamba
“Nikitaka kutoka nje, naweza hata muda wa kawaida hivyo nikichelewa haina maana na-cheat”
uwe makini na huo usemi kwani ukweli ni kwamba wanaume wengi hutumia muda wa ziada na si muda wa kazi kufanya cheating zao.
Ukiona mume ana dalili za kukwepa kuwepo nyumbani kama ilivyokuwa kawaida, basi inabidi uwe makini na kuchunguza kujua nini kinaendelea.

NINI CHA KUFANYA:
Ni vizuri kukaa pamoja na kujadili pamoja kuangalia kama kuna issues ambazo haridhiki nazo zirekebishwe haraka ili arudi kwenye mstari.

Pia jiulize:
Je, hapo nyumbani kuna amani, heshima, upendo, na utulivu?
Na je, namna unaongea na mume wako kuna respect? Au ni kulalamika, hasira, huzuni na yeye anajiona ni failure na loser?
Inawezekana huko anaenda kunampa kile anakikosa hapo nyumbani au kwako wewe mke.

2. TENDO LA NDOA MARA CHACHE
Kupunguza kwa kiwango cha sex kati ya mke na mume ni dalili mojawapo kwamba kuna kitu hakipo sahihi na mojawapo inaweza kuwa mume anachepuka kwa “yule mwanamke”.
Pia unaweza kuijua hii dalili mapema na ukazuia huzuni kutokea katika ndoa yako kwa kupiga gia ya reverse kwa kuongeza frequency za sex kati yako na mumeo.
Wapo ambao ni wajanja zaidi ambao huendelea na sex kama kawaida ili wasishtukiwe hata hivyo kutokana na kuwekeza kwa “yule mwanamke” automatically akiwa na mke wake hamu hupungua na matokeo ni kupungua kwa uhitaji na kiwango cha sex hushuka.

NINI CHA KUFANYA:
Kwanza jiulize swali hili:
Je, kiwango cha sex ni mara chache kuliko kawaida? Kama ni chini ya kiwango ni vizuri wewe mwanamke pia kulianzisha uone nini kinatokea.
Kama mwanamke Jitahidi kutengeneza mazingira ambayo yatakufanya usijisikie kuchoka sana na kama inawezekana unaweza kumuomba mume wako kukusaidia kazi ndogondogo za pale nyumbani.
Pia fikiria ni kitu gani unaweza kuongeza (kipya) ili kuimarisha sex na kama inawezekana mnaweza kwenda nje ya hapo nyumbani kwa ajili ya kuwa na intimacy zaidi.

3. ANAANZA KUKUKWEPA WEWE MWENYEWE MKE WAKE
Anaweza kukukwepa kwa njia zile mnatumia kuwasiliana iwe mchana au usiku huanza kupunguza.
Unaweza kujikuta simu hazijibiwi, sms hazipewi majibu na mara simu imefungwa.
Kama ana simu ya mkononi anaanza kutembea nayo hadi anapenda kuoga, anapoi-charge kama ni nyumbani basi ataisimamia kama FBI wanaomsimamia terrorist aliyekamatwa kabla ya kujilipua.
Na kuna simu akiipokea No matter what ataenda kuongelea nje au kwenye uchochoro wowote.
Kama upo makini utajua tu something is not right!
Kikubwa zaidi hapendi kuwa na wewe “closer” kitendo hiki hufanya muwe mbali kihisia.

NINI CHA KUFANYA:
Jaribu kuchunguza kama simu unazompigia sinamsumbua kazini au ni jeuri yake tu na ukorofi kwa sababu ya “yule mwanamke”
Ongea naye namna ya kuwa na muda pamoja kwa kila wiki.
Wakati mwingine mpigie simu ya kumpa appreciation kwa ajili ya kitu chochote amefanya badala ya simu za kulalamika na kumfanya ajione failure na loser.
Kama una hints chunguza simu yake ya mkononi na kama huna hints achana nayo kwani hakuna mwanaume anapenda kutembea huku amefugwa video camera usoni kuchunguzwa kila kona anayopita.

4. ANAKUWA CRITICAL
Alikuwa anapenda mapishi yako, unavyoonekana (sura na maumbile), mapenzi yako, namna unapenda bajeti; ghafla from nowhere anaanza kulalamika na kukulaumu kwa kila unachofanya.
Inawezekana tatizo ni yule mwanamke!
Kiti kidogo kikikosewa inakuwa kama kapatia sababu ya kuanzisha mgogoro au vita ya tatu ya dunia.
Wakati mwingine anaweza kuwa mwonezi.

NINI KIFANYIKE:
Jadili kwa nini mume wako anakuwa critical na wewe muulize kwa upendo bila wewe kuwa critical pia.
Pia jadili kujua tatizo lipo wapi ili lirekebishwe huku wote mkiwa positive.




NINI MWANAMKE UHITAJI?

NINI MWANAMKE UHITAJI?


Naitwa sixberty Manson 
Kwa maoni na ushauri : 0714 823432






Ili Mke awe available kwa mume kimwili na kiroho inampasa mume awe na sifa zifuatazo:

Ukaribu, uwazi katika mambo yake, anayeeleweka, mtu wa amani, anayempa uhakika mke kwamba ni yeye peke yake ndiye anapendwa na mume wake na pia kumpa uhakika kwamba yeye ni mwanamke mwenye sifa anazozipenda kimwili (beauty) na kiroho.

Je, unawezaje kuwa mume ambaye mke anakuelewa?

Ili mke akuelewe mume unahitaji kutumia secret weapon ya sikio lako.
Kumsikiliza tu mke huweza kuonesha kwake kwamba umemuelewa kuliko hata kabla hajamaliza kuongea wewe unamkatiza na kusema ulikuwa unajua anataka kusema kitu gani.

Tofauti kubwa ya mwanamke na mwanaume ni kwamba mwanaume kawaida yupo wired kusikilizwa na si kusikiliza, na mara nyingi mwanaume hupenda kutatua tatizo au matatizo au kutoa jibu kwa ajili ya tatizo lolote, hivyo anapoongea na mke wake kwa kutomfahamu anakuwa na haraka ya kutaka kutoa majibu badala ya kusikiliza tu.

Narudia tena;
Si mara zote mwanamke anapouliza swali au kukwambia kitu anahitaji majibu, mara nyingi anakuwa katika harakati ya kujihusanisha (connection) na wewe na anachohitaji ni sikio lako tu na si namna ya kupata majibu.
Unachotakiwa kufanya ni kumsikiliza na kushiriki katika kuzungumzia hiyo shida yake na kuliona kama tatizo lenu wote.

Mwanamke huhitaji mtu wa kumsikiliza tu na sikio lako wewe mume ndilo analihitaji na si uwezo wako wa kutatua tatizo.
Ukimsikiliza, atajisikia vizuri tofauti na ukirukia kukatiza kile anaongea au kuanza kupendekeza solutions kwa kile anakwambia.

Wanaume kujitahidi kutoa solutions za kile mke anaongea au hata kukatiza kile anaongea kwa mume kujifanya anajua mke alitoka kuongea kitu gani ni moja ya matatizo sugu ya kwenye ndoa.
Hata kama wewe ni mwanaume maarufu kutatua matatizo ya wanaume wenzako bado ukiwa na mke wako unatakiwa kumsikiliza tu na sikio lako hadi aridhike.

USALITI WA NDOA

MPENZI  msomaji wangu Naitwa sixberty Manson 
karibu katika safu  ya saikolojia leo, kasi ya kusalitiana kwa wapenzi(wanandoa) wengi siku hizi imekuwa ikiongezeka kila kukicha kiasi kwamba unapoingia katika uhusiano wa kimapenzi unahisi kama unaingia kwenye matatizo makubwa na hii ni sababu watu siyo waaminifu kabisa kwa wapenzi wao. Unaweza kuwa na mpenzi wako ambaye kila mnapoonana anakueleza kuwa, hawezi kukusaliti na atakuwa na wewe katika shida na raha siku zote. 

wapenzi waliogombana
Utafit wa wanasaikolojia umebani uhaminifu,nin silaha kubwa kwa wanandoa (wapenzi), mbali na mila ,tamaduni katika nchi au jamiina mengine.

Lakini hivyo hivyo usishangae siku moja ukamkuta yuko na mtu mwingine. Swali la kujiuliza ni kwamba, kwa nini wanandoa(wapenzi) wanachepuka? suluhu, hiki ndicho nilichopanga kuzungumzia siku  leo. Kwa wanandoa(wapenzi)  nitaainisha baadhi ya mambo ambayo kwa uchunguzi wangu nimebaini ndiyo yanayochangia kuchepuka kwa  wanandoa (wapenzi) walio wengi kuchepuka, wawe wako kwenye ndoa au uhusiano wa kawaida.


sababu ni hizi;

TAMAA ZA KIMWILI NA PESA 
Tamaa hasa ya pesa imekuwa ikiwashawishi watu kushindwa kujizuia kuwasaliti wapenzi wao. Kwa wale ambao wako kwenye ndoa wakati mwingine hasa wanawake wasipopatiwa mahitaji yao muhimu na akatokea jamaa na kumhakikishia kwamba atampatia kila anachotaka, wanakubali mara moja bila kujua kwamba wao ni wake za watu ama wapenzi wa watu na kujikuta wanajenga mazoea. Wengine wanapatiwa kila kitu na waume zao lakini sasa kinachotokea ni tamaa za kimwili tu ambazo zinawasumbua na kujikuta wanatafuta wanaume wengine huku wakidai kuwa wanatafuta ladha tofauti.

Hili si kwa wanawake tu hata wanaume pia, unaweza kumkuta ana mwanamke bomba tu mwenye kila kigezo, lakini bado anakuwa na tamaa za kutafuta kimwana mwingine nje.
TABIA ZISIZORIDHISHA 

Hapa wapo  wale  ambao wanaishi  maisha  ya  ajabu  sana, yaani wanaishi  katika(ndani) ya  ndoa  ama  wapo ndani ya uhusiano  wakielekea kwenye kuoana lakini  hawaaminiani  kabisa,  kila mtu anakuwa  na wasiwasi  juu ya mwenzake.     Afadhali  sasa  iwe kutokuaminiana  tu  lakini hapa  wapenzi  wanakuwa  hawasalitiani. 
Kuna wale ambao  ni  wazi  hawatulii  katika  mahusiano yao, yaani matendo yao (tabia)  tu  yanaonesha  dhahiri kabisa  kwamba, uaminifu  ni sifuri. Kuwa  kari bu sana  na  watu  wa  jinsia tofauti na  tabia ya kuwa na mawasiliano nao ya siri au mwanamke anapomuwekea  mumewe  vikwazo  katika  tendo la ndoa  chumbani (sex) anatarajia  akafanye wapi  na nani?  Kama  siyo kumwambia akatafute   wengine nje?    Hii ndiyo maana  wapenzi wenye tabia wanaowanyima  unyumba waume zao hata wanaposikia  kwamba  wanasalitiwa  wanakuwa hawana  nguvu ya kuwashutumu wapenzi wao, utamshutumuje wakati wewe humtimizii  katika mambo flani? Si hivyo tu, kwa upandea wa wanaume  nao  (baadhi )wengine wamekuwa  wakiwasusa  wake zao na kukaa  siku mbili au wiki na  zaidi  bila kuonekana nyumbani  hata kama atarudi nyumbani  basi  usiku  wa manane akiwa amelewa nawew  hana  mpango kabisa wa mapenzi  na mke wake,katika mazingira hayo  unadhani  nini  kinaweza kutokea kama siyo mwanamke kutafuta mwanaume atakayempatia mapenzi? Na mume kuoa mkee mwengine .
KUWEPO  KWA MAPENZI YA KILAGHAI
(uonngo).
Tunapozungumzia  mapenzi  tunaweza  kuyagawanya  katika makundi mawili, mapenzi ya kweli na mapenzi ya uongo. Walio katika  mahusiani au mapenzi ya kweli huwezi  kuwasikia wamesalitiana. Ila wale walio katika mapenzi ya kudanganyana tabia ya kusalitiana  ni  kitu cha kawaida  kwao na hivyo  kujikuta kila siku wakifumaniana.
UDHAIFU  KWA WAPENZI 

Udhaifu  ambao umezungumziwa  hapa  ni  ule  wa kimaumbile (big dick) ambao hata hivyo na wataalam wa masuala ya mapenzi wanaeleza  kwamba, haiwezi kuchukuliwa kama ni miongoni  mwa  sababu  ya  kumsaliti  mpenzi wako uliyempenda kwa dhati. Kwa mfano, mwanaume unakuwa ‘Functionless’ yaani jogoo hawiki (tatizo ambalo si la kujitakia)  na  mke wake  hayuko tayari kuendelea  kuwa  naye  hivyo kulazimika  kuomba  talaka.  Lakini mwanaume anakuwa  mgumu  wa  kutoa  talaka  kutokana  na jinsi anavyompenda.

Wengi  wao wanachokifanya  ni  kuendelea  kuwa  katika  ndoa huku  wakiangalia uwezekano  wa kuanzisha au kuwa na  uhusiano  na  mtu  mwingine  wa  nje. Kwa wanawake  nao yawezekana kuwa  mwanamke hazai (tatizo  ambalo si la kujitakia pia na mwanaume anahitaji mtoto, atakachokifanya  ni kutoka(kuchepuka) nje ya ndoa yao  kwa siri lakini pia inaweza kufikia hatua mwanamke akagundua. Kwa  kifupi  ni kwamba ni c hanzo, kusalitiana kwa wanandoa  wengi  kumekuwa  kukitokea kutokana na  kuwepo  kwa mazingira fulani  ambayo  hupelekea kuwa  baadhi yao wamekuwa  wakishindwa  kujizuia nayo  na hivyo kujikuta  wanatoka  nje  ya mahusiano yao.

SULUHISHO
Ila sasa  na lazimika kwa nguvu zote  kuwashauri  wale  walio  katika  uhusiano wa kimapenzi, namaanisha  wapenzi wa kawaida, na  wachumba  pamoja  na wanandoa, tusiwe  na tamaa za kijinga na kufikia hatua ya kuwasaliti  wapenzi wetu. Hivi unajisikiaje unapomvulia  nguo  mtu  ambaye wala hana ‘future’ na wewe? Hivi  na wewe ukifanyiwa hivyo  na  mpenzi  wako  utajisikiaje? Sasa elewa yakuwa maumivu utakayoyapata  pale  utakaposikia mpenzi wako ana uhusiano  na  Fulani  ni hayohayo atakayoyasikia mwenza (mpenzi)  wako.
NI  kuwa  muaminifu, kuridhika  na unachokipata  kwake, muoneshe mapenzi ya dhati naye  atafanya hivyohivyo  na wote kujikuta  mnayafurahia  maisha yenu. Mfano, jadilini na kutatua matatizoyenu, kwa  pamoja  mipango  yenu ya familia, maendeleo, hali inayoleta mapenzi yenu  kuwa na furaha  na kulinda ndoa.

 

SIXBERTY MANSON POSTS

Mona Lisa

  MONALISA                              LA GIOCONDA                          By Sixberty Manson  A picture by Sixberty Manson  MEET THE REAL...

ZILIZOTAZAMWA ZAIDI